TANZANIA NI NCHI YA 9 KWA UCHANGIAJI MKUBWA WA ASKARI KATIKA ULINZI WA AMANI WA UMOJA WA MATAIFA







Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametumia Siku ya leo na Walinzi wa Amani wa Umoja wa Mataifa nchini Mali ili kuonesha mshikamano wake na watu wanaokabiliwa na hatari kubwa ya kifo na hali tete  katika kuadhimisha miaka 70 ya Ulinzi wa Amani wa Umoja wa Mataifa.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotumwa kwa vyombo vya habari Bwana Guterres amesema kuwa umoja wa maifa unatoa shukrani kwa wanaume na wanawake zaidi ya milioni moja ambao wametumika chini ya bendera ya Umoja wa Mataifa kuokoa maisha ya watu wengi ikiwa ni pamoja na kuwaenzi askari wenye kofia za samawati zaidi 3,700 ambao  walipoteza maisha yao katika miongo saba iliyopita. 

Amefafanua kuwa wakati wa migogoro isiyoelezeka na kuongezeka kwa vifo vya walinzi wa amani anatambua  huduma ya kujitolea duniani kote hivyo  ameahidi kuchukua Hatua kwa ajili ya Walinzi wa Amani kwa  kufanya operesheni zao kuwa madhubuti na salama zaidi katika mazingira ya sasa yenye changamoto.

Aidha atakaporejea kutoka Mali Bwana Getteres ataongoza maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Walinzi wa Amani kwenye Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York siku ya Ijumaa, tarehe 1 Juni ambapo ataweka shada la maua kuwaenzi wale wote waliopoteza maisha yao katika huduma ya amani na pia ataongoza sherehe ya kutunuku Medali kwa watumishi 129 wa kijeshi, polisi na raia waliopoteza maisha yao katika operesheni za kulinda amani mwaka 2017 moiongoni mwao wakiwa walinzi   20 kutoka Tanzania.

Tanzania ni nchi ya 9 kwa uchangiaji mkubwa wa askari katika Ulinzi wa Amani wa Umoja wa Mataifa ambapo hivi sasa inachangia karibu wanajeshi na polisi 2,700 kwenye operesheni za ulinzi wa amani huko Abyei, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Lebanon, Sudan pamoja Sudan Kusini.

Jean-Pierre Lacroix Katibu Mkuu Msaidizi anayesimamia Operesheni za Ulinzi wa Amani mashinani amesema kuwa Walinzi wa amani wa umoja wa mataifa wanaokoa maisha kila siku ambapo Leo  wanawaenzi wale waliotoa mhanga maisha yao kwani kujitolea kwao  kunawahamasisha kufanya kazi kwa bidii zaidi ili kusaidia amani endelevu katika  maeneo yenye changamoto nyingi.

SOURCE.TRIPLE AFM/ARUSHA

No comments

Powered by Blogger.