MAONESHO YA MIFUGO NA KONGAMANO LA WIKI YA MAZIWA YAANZA ARUSHA.




Mkuu wa wilaya ya Arusha Gabriel Daqwaro amewataka wananchi wa Mkoa wa Arusha kujitokeza kwa wingi katika kutembelea Maonesho ya Mifugo na Kongamano la wiki ya maziwa katika viwanja vya nanenane Njiro Mkoani hapa ili kuweza kupata elimu juu ya unywaji wa maziwa na kujua teknolojia mbalimbali za ufugaji kwa lengo la kufuga kwa tija.

Akiongea na waandishi wa habari Daqaro kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha amesema kuwa Mkoa kwa kushirikiana na baraza la kilimo taifa pamoja na bodi ya maziwa wameamdaa maonesho kitaifa ya kwanza ya  Mifugo na maadhimisho ya 21 wiki ya maziwa kwa lengo la kujenga ubia wa kibiashara  na mtandao.

Amefafanua kuwa malengo mengine ya Maonesho hayo ni kubadishana ujuzi ,teknolojia na uzoefu, kutafuta fursa za masoko miongoni mwa wadau pamoja na kuainisha fursa na kushawishi uwekezaji katika sekta ya Mifug.

Source.triple a fm/arusha

No comments

Powered by Blogger.