WAMAREKANI WASAIDIA KUKUZA TEHAMA ARUSHA DC
Shule 10 za sekondari kati 27 za halmashauri ya Arusha zimenufaika na mradi wa tehama kwa kupewa zaidi ya kompyuta 20 kwa kila shule zinazosaidia walimu katika kufundisha na wanafunzi kujifunza.
Mratibu wa mradi huo ambaye pia ni afisa tehama wa
halmashauri hiyo David Nyangaka amesema kuwa kompyuta hizo zimetolewa na
wafadhili kutoka Marekani na zimekuwa msaada mkubwa katika elimu ndani
ya halmashauri hiyo.
Mkurugenzi wa halmashauri hiyo Dokta Wilson Charles Mahera
amesema kuwa shirika hilo limeahidi kuongeza kompyuta hizo kwa shule
tatu ambapo wamependekeza ziende katika shule ya Kimnyak, Kiranyi na
Sokon two.
Adam Namama Mwalimu wa kompyuta katika Sule ya sekondari
Mringa amesema kuwa shule yao ina kompyuta 24 na wanazitumia kwa
manufaa ya walimu na wanafunzi ambapo wote kwa pamoja wanazitumia kwa
kutafuta matirio ya masomo mbalimbali ya kujifunzia na kufundisha.
Mwanafunzi wa shule hiyo kutoka kidato cha pili na cha tatu
Recho Aron, David Smoke na Floriana Amedeus wameeleza kuwa kompyuta
hizo zinawasaidia kupata vitabu mbalimbali vinavyowasaidia kusoma vizuri
ikiwa ni pamoja na kupata ujuzi utakao wasaidia baada ya kuhitimu.
Source.tripleafm habari machi 04 2018

Post a Comment