KONGAMANO LA BIBI NI NGUZO LAACHA GUMZO ARUSHA


 

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mgwira ametoa wito kwa halmashauri zote hapa chini kuangalia uwezekano wa kuwapa wazee bima  ya afya pamoja na kuwapa kipaumbele katika mgao wa fedha za miradi ya vijana na wanawake zinazotokana na asilimia 10 ya mapato ya ndani.

Bi Mgwira ametoa wito  huo Leo wakati akifunga Kongamano la wabibi lililofanyika Mkoani Arusha ambapo amesema kuwa maisha ya wabibi wengi hayana akiba,malipo ya uzeeni wala fidia ya majanga hivyo halmashauri ziwape kipaumbele.
Bibi Edith Tarimo mshiriki wa Kongamano hilo  amesema kuwa tangu  virusi vya ukimwi viingie nchini wabibi wamekuwa wakiwalea watoto wa watoto wao waliofariki dunia kutokana na ugonjwa huo ambapo bibi mmoja analea wajukuu wanne hadi 10 jambo ambalo  sio jepesi kwao.
Hata hivyo Kongamano hilo  lililowashirikisha wabibi  250 kutoka Mkoa ya Tanzania na 40 kutoka nchi za nje  umebeba kauli mbiu isemayo  "bibi ni nguzo" ambapo umehitimishwa kwa maandamano ya amani  yaliyoendanda sambamba na ubebaji wa mabango yanashinikiza kutengewa Siku maalum ya wabibi nchini. 
 
Source.tripleafm habari Machi 04 2018








No comments

Powered by Blogger.