TASAF AWAMU YA TATU YAKUMBUSHWA KUWAFIKIA WALENGWA HALISI
Baadhi
ya wazee kutoka katika mikoa mbalimbali hapa nchini wameilalamikia
serikali juu ya mradi wa kunusuru kaya masikini Tasaf awamu ya Tatu
kutokuwafikia watu Mwenye mahitaji maalum badala yake kuwafikia watu
wenye nguvu za kufanya kazi.
Akizungumza na waandishi wa habari bibi Christin Mahenga
kutoka dar-es-saalam katika Kongamano la akina bibi lililofanyika Arusha
amesema kuwa mradi huo umekuwa ukiwafikia watu wanaoshindwa
kujishughulisha kwasababu ya uvivu na kuwaacha wazee wasiojiweza bila
msaada.
Jane Marigo bibi kutoka Arusha amesema pamoja na serikali
kuwasaidia wazee kupata matibabu bure bado wanaiomba iwasaidie fedha za
kujikimu kupitia mradi wa Tasaf ili waweze kuanzisha mradi itayowasaidia
kuwaleo wajukuu walioachwa na wazazi wao kwa kufariki dunia na kupata
lishe itayowaimarisha.
Kwa upande wake Tajiaeli Mahega mratibu wa Tasaf Jiji la
Arusha amefafanua kuwa walengwa wanaohusika na malipo ya kaya masikini
ni wale wanaoahindwa kupata Milo mitatu kwa Siku na vigezo vingine
vinawekwa na wananchi katika maeneo yao.
Source.tripleafm habari machi 4 2018
Post a Comment