BODABODA JENGENI HESHIMA YENU-MWIGULU



Waziri wa mambo ya ndani Dokta Mwigulu Nchemba amewataka madereva bodaboda kote nchini kufanya kazi ya bodaboda kuwa ya heshma kutokana na kazi hiyo kuleta maendeleo makubwa kwa nchi kwa kurahisisha utoaji wa huduma na na upatikanaji wa ajira kwa vijana.

Mwigulu ametoa wito  huo wakati akizungumza na madereva bodaboda Mkoani Arusha baada ya kusikiliza taarifa  ya marejesho ya mkopo wa pikipiki uliotolewa kwa madereva bodaboda wa kata 25 za wilaya ya Arusha ambapo amesema kuwa;bodaboda ni hatua  kubwa ya mafanikio ya nchi hivyo wanapaswa kujivunia na kufanya shughuli ya heshima na sio shughuli inayofanywa na watu waliokosa kazi za kufanya.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho  Gambo ameeleza kuwa walifikia utaratibu wa kutoa  bodaboda miambili zenye thamani ya millioni mianne baada ya kuona kuwa madereva bodaboda ni watu ambao  hawawezi kupata fursa za kukopa  kwenye mabenki kutokana na kutokidhi vigezo na masharti.

Naye Mwenyekiti wa umoja wa madereva wa bodaboda Jiji la Arusha (UBOJA)  Bwana Maulid Makongoro ameeleza  kuwa kwa sasa umoja huo una wanachama elfu tano ambapo walipata fursa ya utatuzi wa changamoto ya mitaji iliyokuwa ikiwakabili kwa kupata mkopo wa usio na riba wa pikipiki mia Mbili kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho  Gambo.

Bwana Makongoro ameeleza pikipiki hizo ziligawanywa kwa uwiano sawa kwa kata zote 25 za Jiji la  Arusha ambapo kila kata walipata pikipiki 8 na hadi sasa wamefanya marejesho ya zaidi ya millioni  mia tatu.

Source.tripleafm/habari machi 4 2018

No comments

Powered by Blogger.