SOKONI TWO ARUSHA WAFANYA HARAMBEE ILI KUTATUA CHANGAMOTO YA MAJI
ARUSHA
Wananchi wa Kijiji cha Sokoni Two Kata ya Sokon Two katika
Halmashauri ya Arusha wamefanya harambee kwa ajili ya kutatua
changamoto ya maji katika kijiji chao.
Bi Miriam Mosesi ambaye ni mkazi wa kijiji hicho
ameeleza kuwa endapo watafanikiwa kutatua changamoto hiyo itawawezesha akina
mama kufanya shughuli mbalimbali za maendeleo kwani muda mrefu wanautumia
kutafuta maji.
Ka upande wake Mwenyekiti wa kijiji hicho Bwana Obedi Melami amesema
kijiji hicho chenye vitongoji vitano kinakabiliwa na changamoto ya upungufu wa
maji kutoka na maji wanayoyapata kutoka kijiji cha jirani kuhujumiwa na watu
wenye mashamba makubwa.
Naye OLTESH Thobias ambaye ni mkazi wa kijiji hicho
amesema changamoto kubwa inayosababisha maji yasifike katika kijiji hicho ni
miundombinu; hivyo wameweza kupata zaidi ya milioni saba zitakazowezesha
kuboresha miundombinu hiyo ili maji yapatikane.
Akiwa katika ziara yake ya kikazi mkoani Mwanza; hivi
karibuni Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alisema serikali kupitia Kampeni ya Rais
Dokta John Magufuli ya kumtua mama ndoo, itahakikisha wananchi katika maeneo
yote nchini watapata huduma ya maji safi na salama katika umbali usiozidi mita
400 kutoka kwenye makazi yao.
Source.tripleafm news/27.02.2018

Post a Comment