MPANGO WA KUWAWEZESHA WAZEE KUPATA HUDUMA ZA AFYA BURE UPO PALEPALE-RC GAMBO
ARUSHA.
Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amesema serikali ina
mpango kuwatambua wazee wote nchini ili waweze kupata vitambulisho
vitakavyowasaidia kupata huduma za afya kwa kadri sheria, taratibu na sera za
nchi zitakavyo ruhusu.
Gambo amesema hayo jijini Arusha wakati akifungua
kongamano la tatu Afrika la Akinabibi wanaolea wajukuu ambao wazazi wao
wamefariki dunia ambapo ameeleza kuwa mpango huo utawasaidia kupata takwimu sahihi
za akinabibi hao katika ngazi ya kijiji hadi mkoa ili kuweza kupeleka huduma
mbalimbali kwao ikiwemo huduma ya afya.
Kwa upande wake Ndinini Kimesera mkurugenzi wa shirika
linalojishughulisha na masuala ya maendeleo ya wanawake wa kimasai(MWEDO) amesema
lengo kubwa la kongamano hilo ni kutambua nafasi ya bibi katika janga la Ukimwi
hasa kwa kuwalea na kuwatunza wajukuu wao walioachwa na wazazi wao.
Christina David bibi kutoka Kimara jijini Dar-es-salaam
ameeleza kuwa pamoja na serikali kuwaletea huduma ya elimu bure bado
wanakabiliwa na changamoto nyingi katika kuwalea wajuu kwa kushindwa
kuwatimizia mahitaji mengine kama vile matibabu, sare za shule, madaftari
pamoja na huduma nyingine muhimu.
Source.triplea fm habari/27.02.2018

Post a Comment