BAADHI YA KAYA ZAONA MANUFAA YA TASAF AWAMU YA TATU ARUSHA
ARUSHA.
Baadhi ya wanufaika wa mradi wa TASAF awamu ya Tatu
jijini Arusha wameishukuru serikali kwa kuwaletea mpango huo kwani umewasaidia
kujikwamua kiuchumi na kuendesha maisha yao ya kila siku.
Wanufaika hao wametoa shukrani zao kwa Katibu wa Itikadi
na Uenezi Taifa CCM, Humphrey Polepole aliyekuwa katika ziara ya kikazi ya
ukaguzi wa miradi ya maendeleo ya TASAF ambayo ni sehemu ya utekelezaji wa
ilani ya CCM.
Wamesema mradi huo umebadilisha maisha yao tofauti na
awali kwani kwa sasa wanawezan kupata milo mitatu kwa siku, watoto kwenda
shule, pamoja na kufanya biashara mbalimbali zinazowaingizia kipato.
Akisoma taarifa ya utekelezaji wa miradi mbalimbli ya
TASAF Mratibu wa TASAF jiji la Arusha Tajiel Mahega amesema asilimia kubwa ya
kaya maskini hizo tayari wamesha patiwa kadi kwa ajili ya matibabu (Tika) yenye
uwezo wa kuhudumia kaya sita kwa kadi moja.
Katibu wa Itikadi na Uenezi Taifa CCM, Humphrey Polepole
ameagiza wasimamizi wa Mpango wa kunusuru kaya masikini na zenye upungufu wa
chakula TASAF mkoa wa Arusha kufanya tathmini na kuongeza ruzuku kaya
zinazofanya maendeleo ili kuongeza uzalishaji ili kuwa chachu ya maendeleo
katika jamii.
Source.triple a fm habari/27.02.2018

Post a Comment