"HARAKISHENI MRADI WA MAJI WA WB TUPATE MAJI"WANANCHI LIKAMBA






ARUSHA.

Wananchi wa kata ya Musa kijiji cha Likamba Wilayani Arumeru wameiomba serikali kuharakisha utekelezaji wa mradi wa maji wa benki ya dunia uliosimama kwa muda mrefu ili waweze kupata huduma ya maji safi na salama kwani hutumia muda mwingi kutafuta maji kuliko kufanya shughuli za maendeleo.

Bi Evaline Abel mkazi wa kitongoji cha Olomponi amesema tatizo la ukosefu wa maji limewafanya wanawake katika kata hiyo kushindwa kufanya shughuli za maendeleo kutokana na kutumia muda mwingi kutafuta maji na mara nyingine watoto hawaendi shule

Samwel Satian mkazi wa kitongoji cha Olomishira ameeleza kuwa wamekuwa wakifuatilia utekelezaji wa mradi huo katika ngazi mbalimbali za wilaya hiyo lakini bado hakuna kunachoendelea hali inayowanyima kuchangamkia fursa za maendeleo zilizopo katika kilimo na ufugaji. 

Akizungumzia kuhusiana na utekelezaji wa mradi huo Diwani wa kata hiyo Bi Flora Zelote amesema unatekelezwa katika vijiji vitatu na katika kijiji cha Likamba umekamilika kwa asilimia 60.

Utekelezwaji mradi huo ulianza toka mwaka 2013 lakini mpaka sasa bado haujakamilika; huku wananchi wakiendelea kukabiliwa na changamoto ya ukosefu wa maji.

sOURCE.TRIPLEA FM HABARI/27.02.2018

No comments

Powered by Blogger.