SERIKALI YAOMBWA KUSIKIA KILIO CHA HUDUMA DUNI ZA AFYA OLDONYO SAMBU
ARUSHA.
Kufuatia kukabiliwa na changamoto za Afya ikiwemo
ukosefu wa Wauguzi katika zahanati ya Oldonyo Sambu,pamoja na kutembea umbali
mrefu kufuata huduma za Afya wananchi katika kijiji cha Oldonyo Sambu Wilaya
ya Arusha wameiomba serikali kusikia kilio kwa kuzipatia ufumbuzi
changamoto hizo.
Wakizungumza na triple A fm baadhi ya akina mama hao
waliofika kupata huduma katika zahanati hiyo wamesema haina vifaa tiba vya
kutosha na pia ina muuguzi mmoja hivyo kushindwa kuhudumia wagonjwa wengi kwa
wakati mmoja.
Wamesema umbali mrefu umekuwa ukisababisha adha kubwa
hususani kwa akina mama wajawazito pindi wanapotaka kuhudhuria clinic kwa
wakati na hata kina mama wengine hushikwa na uchungu wakiwa njiani kwenda
kujifungua
Bwana Piniely Meyasi amesema Zahanati hiyo inakabiliwa
na changamoto ya uhaba wa majengo,umeme
pamoja na maji safi na salama
hivyo ameiomba serikali kutatua
changamoto hizo mapema ili kuzuia athari zisiendelee kujitokeza
Muuguzi wa zahanati hiyo ambaye amekataa kutaja jina lake amekiri kuwepo kwa
changamoto hizo katika zahanati hiyo na
kusema inategemewa sana kwani asilimia 80 ya wakazi wa kijiji hicho na vijiji vya jirani wanapatiwa huduma za afya hapo.
Pamoja na jitihada za serikali kupitia sekta ya afya
kuwasisitiza akina mama wajawazito kuhudhuria clinic kwa wakati na kutojifungulia
majumbani baadhi ya maeneo ya pembezoni utekelezaji wake bado ni changamoto.
Source.triple a fm habari/27.02.2018

Post a Comment