Serikali kufuta utitiri wa mifuko hifadhi ya jamii
Magufuli amesema Serikali ina mpango wa kufuta utitiri wa
mifuko ya hifadhi ya jamii na kubakiza miwili.
Amesema mifuko itakayobaki ni kwa ajili ya kuhudumia
wafanyakazi wa sekta binafsi na ya umma.
Rais Magufuli amesema Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii
(NSSF) litabaki kwa ajili ya kuhudumia wafanyakazi wa sekta binafsi wakati
mifuko mingine yote itaunganishwa na kuwa mmoja.
Amesema hayo leo Alhamisi Desemba 14,2017 alipofungua
mkutano mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) mjini Dodoma.
Mifuko mingine inayotoa huduma ya hifadhi ya jamii ni PSPF,
LAPF, PPF na GEPF.
Rais Magufuli amesema baadhi ya mifuko ya hifadhi ya jamii
imekuwa haiwasaidii wafanyakazi badala yake imekuwa ikiwekeza kwenye ujenzi wa
majengo makubwa
Mifuko hii haiwanufaishi wafanyakazi bali wapiga dili ambao
huamua majengo yajengwe na wao kupata asilimia 10,” amesema.

Post a Comment