BREAKING: Askari Magereza Arusha amuua askari mwenzie kwa risasi

Polisi inamshikilia kwa mahojiano askari Magereza wa Gereza la Kisongo jijini Arusha, Koplo Faustine Masanja kwa tuhuma za kumuua mwenzake wakiwa kazini.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo amethibitisha tukio hilo lililotokea leo Alhamisi Desemba 14,2017 asubuhi

Amesema baada ya Masanja kumjeruhi mwenzake Koplo Ombeni kwa risasi, alipelekwa hospitalini kwa ajili ya matibabu ambako alifariki dunia

Kamanda Mkumbo ameahidi kutoa taarifa zaidi baada ya uchunguzi kukamilika ili kubaini chanzo na sababu za tukio hilo

Hata hivyo, taarifa zinadai huenda chanzo cha shambulio hilo kikawa ni wivu wa mapenzi

No comments

Powered by Blogger.