Tetesi za soka Ulaya Jumatatu 20.11.2017

Manchester City itashindana na Liverpool kumununua beki wa Southampton na Uholanzi Virgil van Dijk, 26, katika dirisha la uhamisho la Januari.{Daily Mirror}.
City pia inataka kumsajili kiungo wa kati wa Schalke na Ujerumani Leon Goretzka ambaye kandarasi yake inakamilika mwishoni mwa msimu huu na amewavutia Arsenal, Liverpool na Chelsea (Daily Mirror)
Mshambuliaji wa Uingereza na Tottenham Harry Kane, 24, anasema kuwa anapanga kuichezea Tottenham kwa kipindi chote cha mchezo wake kilichosalia (London Evening Standard)

No comments

Powered by Blogger.