ManCity, Liverpool na Chelsea zawika Epl

Manchester City ilionyesha mchezo mwengine mzuri katika ushindi dhidi ya Leicester ambao umeimarisha uongozi wake katika kilele cha jedwali la ligi ya Uingereza.

Kikosi cha Pep Guradiola kiliendeleza msururu wake wa matokeo mazuri baada ya likizo ya mechi za kimataifa kwa kujipatia ushindi wa 16 mfululizo katika mashindano yote kupitia uongozi wa mshambuliaji wao Gabriel Jesus kabla ya kiungo wa kati De Bryuine kufunga mkwaju mkali ambao kipa wa Leicester alishindwa kuuona.

Wakati huohuo mabingwa watetezi Chelsea walipata ushindi rahisi dhidi ya West Brom na kumuongezea presha kocha wa West Brom Tony Pulis.

Alvaro Morata alifunga bao lake la nane katika ligi baada ya kufunga mpira uliopanguliwa na kipa Ben Foster kufuatia shambulio la Eden Harzard.

No comments

Powered by Blogger.