KUNA MAWAKILI WENGI MIJINI WAKATI VIJIJINI WANANCHI WAKIKOSA MSAADA WA KISHERIA-JAJI MKUU




ARUSHA.
Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Profesa Ibrahimu Hamis Juma Amewataka Watendaji wa Mahakama Kote Nchini kuhakikisha Wanatoa Nakala za Hukumu kwa Wakati ili Kuondoa Adha kubwa ya Wananchi wanaokufatilia Kesi Mahakamani.

Akizungumza Katika kikao cha Menijementi ya Mahakama kilichofanyika Mkoani Arusha na kukutanisha watumishi ngazi za Mahakama za wilaya 52  kutoka kanda ya kusini, kaskazini, kati lengo likiwa ni kufanya Tathimini ya Mpango mikakati ya Miaka 5  Ijayo.

Profesa Ibrahimu amesema ni muhimu kwa Watendaji wa  Mahakama Kufanya Tathimini ya Mipango kazi pamoja na uwepo wa mikakati Thabiti itakayo weza kujenga mfumo imara na kuondokana na uwepo wa makosa madogo madogo ambayo yanasababisha  udhaifu ,Jambo ambalo amewataka Majaji na Mahakimu  wakati wa usikilizaji wa  mashauri Mbalimbal kutoa Hukumu kwa wakati .

Pia ameongeza kuwa kumekuwepo na mawakili wengi mijiini jambo ambalo Wananchi waliopo vijiijini wanashindwa kupata msaada nakusisitiza kuwa ni vyema kukawepo na Usawa pande Zote ili kufanikisha Huduma na kuongeza hari ya kuwatumikia Wananchi.

Kwa Upande wake Mtendaji  Mkuu wa Mahakama Hussein Katanga  amesema Mahakama inajukumu la kufanya maboresho katika utendaji kazi wake lengo likiwa nikufanya maboresho Katika Mahakama za mwanzo na kutoa haki na ufumbuzi Katika maeneo machache  na  kurudisha Imani ya Wananchi kuiamin Mahakama.

Kwa Upande wake  Mkuu wa kitengo cha maboresho Zahara  Maruma amesema malengo ya maboresho Kwa mwaka 2020_2025 ni kuhakikisha wanayafikia maeneo 17 ya Mipango mikakati waliyojiwekea na  kutimiza  Nguzo ya Utawala bora na namna ya  kuboresha  Mifumo ya Taasisi zakimahakama kama Dira ya Utoaji wa  haki  sawa kwa Watu wote.

source.tripleafm habari-machi 8 2018

No comments

Powered by Blogger.