WABUNGE WA AFRIKA MASHARIKI WAAPISHWA
Wabunge
54 wa bunge la jumuiya ya Afrika mashariki leo wameapishwa rasmi kuwa wabunge
wa jumuiya hiyo ili kuweza kuwakilisha nchi zao katika bunge hilo katika
kutatua masuala mbalimbali ya kimaendeleo.
Kwa
kawaida bunge la jumuiya ya Afrika Mashariki huongozwa katika kipindi cha miaka
mitano kwa wabunge na kisha kufanyika uchaguzi wa kuwateua wabunge wa
wawakilishi kutoka katika nchi tano ikiwemo Uganda,Rwanda,Kenya,Tanzania na
Burundi ambapo nchi ya South Sudan kwa mara ya kwanza ndiyo inaingia katika
bunge la jumuiya baada ya wakuu wan chi kukubaliana mwaka jana kuwa South Sudan
kuwa katika umoja wan chi za afrika mashariki.
Baadhi
ya wabunge wa bunge la Afrika mashariki kutoka nchini Tanzania wakapata wasaa
wakuelezea namna walivyojipanga katika kuhakikisha wanawapa wananchi wa jumuiya
ya Afrika Masharikikipaumbele katika kutatua changamoto zao.
Baadhi
ya wabunge kutoka South Sudan ,Kenya na Uganda wanasema kuwa ni jukumu lao
kuhakikisha wanaweka sawa mambo ya soko la pamoja pamoja na mambo mengine
wanawakilisha nchi zao hivyo ni vyema kama kila mmoja akajiandaa kutimiza wajibu
wake katika bunge hilo ambalo wengi ni vijana.
Lakini
kama nchi ya Tanzania kwa niaba ya spika wa bunge la jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mussa Azan Zungu ambaye ni mwenyekiti wa bunge la Tanzania anasema
kuwa wana hari kubwa na bunge hilo na kwamba wabunge wasijiingize katika
makundi ya ushabiki na badala yake wafanye kazi kwa maadili ili kufanikiwa
katika shughuli zao za kibunge.
Hata
hivyo katika zoezi hilo la viapo kwa wabunge hao limeambatana na uchaguzi wa
spika ambao utafanyika hapo baadae na kwamba wanatarajia bunge hilo kuongozwa
na spika wa Tanzania Adam Kimbisa.

Post a Comment