MSEMAJI WA SERIKALI AZUNGUMZIA SUALA LA KUKATIKA KWA UMEME
Mkurugenzi wa idara ya habari maelezo Dokta Hassani Abbas ametolea ufafanuzi suala la kukatika kwa umeme mara kwa mara jijini Arusha, kwa kuwatoa hofu wananchi kwamba serikali imeanza kuchukua hatua kwa kuongeza uzalishaji wa nishati hiyo pamoja na kufanyia kazi changamoto ya mifumo ya usafirishaji.
Akizungumza katika kipindi maalumu kilichorushwa na kituo cha utangazaji cha Radio Triple A leo Dokta Abasi ametaja miongoni mwa changamoto ambazo zinachangia hali hiyo kwa miaka mingi ni pamoja na kutegemea umeme wa maji pamoja na mabadiliko ya tabia ya nchi.
Amesema kwa kuliona hilo serikali imeanzisha mikakati ya kulipatia ufumbuzi kwa kuongeza vyanzo vya uzalishaji nishati ya umeme ikiwemo miradi mikubwa ya umeme unaotokana na gesi ya kinyerezi one megawatt 150 ambazo zimeingia kwenye grid ya taifa
Amesema Kuna mradi wa upanuzi wa mtambo huo huo wa Kinyerezi one Kinyerezi One Extension ambao unatarajia kukamilika mwaka huu ambapo utazalisha umeme mwingine wa megawatt 135.
Pia amesema Serikali imeanza kujenga mtambo wa Kinyerezi 11 ambao umeshafikia kiwango cha kukamilika cha asilimia 90 ambapo utaongeza umeme kwenye Grid ya taifa Megawatt 240 na mpaka sasa kuna megawatt 112 zinazalishwa.
Pia amezungumzia mradi mwingine mkubwa wa kihistoria wa uzalishaji umeme wa Stieglers Gorge ambao unatarajia kuzalisha umeme wa megawatt 2100 ambao unaenda kuifanya Tanzania kuwa mzalishaji wa nishati ya umeme kwa ajili ya mataifa ya jirani.
Aidha Dokta Abas ameongeza kuwa serikali imeanza kufanyia kazi changamoto ya mifumo ya usafirishaji wa nishati ya umeme kwani kukatika kwa umeme kwa sasa kunachangiwa na mifumo ya umeme na siyo upungufu wa nishati hiyo.

Borgata Hotel Casino & Spa - Mapyro
ReplyDeleteMapYRO users can download the 대전광역 출장마사지 app to their mobile device, 포천 출장샵 using the app's location, 군포 출장샵 address, and computer. Use the 서귀포 출장샵 map to locate the places in the casino 고양 출장샵 and